Thursday, May 10, 2012

TANZANIA INSTITUTE OF FOOD SCIENCE AND TECHNOLOGY


Tanzania Institute of food Science and technology ni taasisi ambayo imeundwa kutoka kwenye chama kilichokuwa kikiitwa Tanzania association of food scientists and technologists ambacho kiliundwa mnamo mwaka 1993. TIFST imeanzindiliwa rasmi tarehe 13th April 2012 na Mheshimiwa katibu wa wizara ya viwanda na biashara Bi Joyce Mapunjo, Ikijumuisha wajumbe mbalimbali kutoka mashirika ya umma na yale ya binafsi kama vile TFDA, TBS, ASAS na SIDO na wanafunzi kutoka chuo kikuu cha kilimo cha sokoine
Tanzania Institute of food science and technology imeanzishwa  baada ya kuona kuwa Tanzania association of food scientists and technologists ni ya kitaaluma zaidi  na ilikuwa haihusishi watu mbalimbali ambao walikuwa wakijihusisha na masuala mbalimbali ya chakula kama vile wasindikaji wadogo wadogo wa  vyakula
Mawazo ya kukianzisha chama hiki cha Tanzania Institute of Food Science and Technology yalianzishwa na DR Anne Perrera ambaye ni mwenyeji wa New Zealand kupitia New Zealand Institute of Food Science and Technology baada ya kufika Tanzania kama mtu wa kujitolea katika fani ya lishe na chakula SIDO Arusha. Baada ya kuwa amefika Tanzania DR Anne akiwa na mwenyeji wake ambaye ni Rose Maeda walifika mpaka Wizara ya mambo ya ndani kuangalia kama kuna chama chochote kile ambacho kimekwisha sajiliwa hapo ofisini ambacho kinajuhusisha na maswala ya chakula, ndipo walipoambiwa habari  ya TAFST. Baada ya maelezo ya kina kutoka ofisi ya msajili wa vyama walibaina kuwa baadhi ya viongozi wa TAFST wapo TFDA na ndipo walipofunga safari mpaka ofisi y a TFDA Kwa Wegenge ili kupata maelezo zaidi. Baada ya kupata maelezo ya kina kutoka kwa Wegenge pamoja na ofisi ya msajili wa vyama waligundua kuwa chama kilikuwa hakiko hai na baada ya kupitia pia katiba yake waligundua kuwa chama hicho yaani TAFST kilikuwa na mapungufu mengi kama vile chama kilikuwa cha kitaluma zaidi na kilikuwa hakiwapi nafasi watu ambao sio wanataaluma wa Sayansi ya chakula na Technologia. Hivyo DR Anne pamoja na Rose Maeda waliuamua kuanzisha mchakato wa kuanzisha chama kipya ambacho kitawajumisha wanataaluma ya sayansi ya chakula na technologia pamoja na wadau mbalimbali wanaojuhusisha na masuala ya chakula kama vile wasindikaji wadogo wadogo wa vyakula pamoja na kampuni kubwa kubwa ambazo zinajihusisha na masuala pia ya chakula. Waliamua kuwasiliana na wadau wachache wanajihusisha na masuala ya chakula kama vile Wahadhili kutoka chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine idara ya chakula ambao ni Prof Tiisekwa, Prof Chove na Prof Laswai pamoja na wadau wengine ambao wameainishwa kwenye katiba. Wadau hawa waliamua kuipitia katiba ya TAFST kwa kina na kubaina mapungufu ambayo yalipelekea wote kwa pamoja kupendekeza na kuamua kuanzishwa kwa Tanzania Institute of Food Science and Technology kwa kutumia malekebisho ya katiba ya TAFST ikiwa ni pamoja na kuzingatia mifumo ya vyama kama hivyo Duniani
Mpaka sasa chama kimeshasajiliwa kwa msajili wa vyama ( MINISTRY OF HOME AFFAIRS) na hakina ofisi lakini kwa sasa wanatumia ofisi za TPSF ambazo ziko Msasani chini ya viongozi wafuatao, m/kiti ni Neema D. Mrema ambaye ni Food technology specialists, na katibu wake ni  Rose Maeda ambaye ni Cluster development specialist.
Chama kitakuwa chini ya usimamizi wa wizara ya viwanda na biashara ingawa mapendekezo yao ya awali ilikuwa chama kiwe chini ya ofisi ya waziri mkuu. Utaratibu wa kutafuta sehemu ya ofisi wizara husika inashughulikia
Wadau ambao walihudhulia kikao ambacho kilifanyika Ubungo plaza walipata fulsa ya kuisoma katiba vizuri na kutoa mapendekezo yao ikiwamo suala la wanafunzi kuingia katika Board of Directors wote kulikubali suala hili. Baada ya mapendekezo na malekebisho mbalimbali kutoka kwa wadau katiba ilipitishwa na ndiyo sasa katiba ambayo inatumika sasa
Chama kwa sasa kiko kwenye michakato ifuatayo;  kujiunga na chama cha sayansi ya chakula na technolojia cha dunia (IUFOST), Usajili wa wanachama katika ngazi tofauti tofauti kama vile zilivyoainishwa kwenye katiba, upatikanaji wa nembo ya chama , kuongeza na kuanzisha vyanzo vya mapato kwa ajili ya shughuli mbalimbali za chama na upangaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo ya chama.
Chama kitakuwa na aina kuu tano za uanachama kama vile zilivyo ainishwa kwenye katiba na kutakuwa na ada  ya uanachama kutokana na ngazi au aina ya uanachama ambao utakuwa nao, na kila mwanachama atatakiwa kujaza fomu za uanachama ikiwa ni pamoja na kufanya shughuli zote za chama .Imeandaliwa na;
Katibu
Elson Backila (0712 733685)
E-mail ; elsonbackila96@upsf.go.tz or elsonbackila@yahoo.com

No comments:

Post a Comment